Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sasa ni zamu ya Dani Olmo kuwapiganisha vigogo Ulaya

Dani Olmo Dani Olmo

Thu, 18 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Barcelona na Manchester City wanaripotiwa kuwa miongoni mwa vilabu vinavyowania kumsajili Dani Olmo wa RB Leipzig na taarifa zinasema tayari timu hizo zimeshafanya mazungumzo na mwakilishi wake.

Fowadi huyo wa RB Leipzig amekuwa bidhaa yenye thamani kutokana na uchezaji wake akiwa na kikosi hicho cha Bundesliga na hasa pia kutokana umahiri wake anapokuwa na timu ya taifa ya Uhispania.

Kulingana na gazeti la Daily Mail, klabu nyingi zimekuwa zikifuatilia nyendo za mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25.

Olmo alisaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Bundesliga Juni mwaka jana utakaoisha mwaka 2027.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live