Tue, 2 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwenyekiti wa Bunge Sports Club and Promotion na Mbunge wa Makete, Festo Sanga amesema kuna haja ya kuwa na mikakati ya nje ya uwanja kwa klabu za Simba na Yanga ili kuibuka na ushindi kwenye mechi za mkondo wa pili za Ligi ya Mabingwa Afrika.
Sanga ameyasema hayo leo Jumanne, Aprili 2, 2024 wakati akizungumza na Mwananchi baada kikao cha kwanza cha mkutano wa 15 wa Bunge la 12 unaoendelea jijini Dodoma ambapo amewataka viongozi wa timu hizo kuungana ili kuhakikisha timu hizo zinapata ushindi kwenye michezo ya marudiano.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live