Winga wa Manchester United, Jadon Sancho amerejea klabuni hapo baada ya mkataba wake wa mkopo na vigogo wa Bundesliga, Borussia Dortmund kumalizika na tayari ameanza mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa 2024/25 akiwa na Manchester United.
Winga wa Manchester United, Jadon Sancho amerejea klabuni hapo baada ya mkataba wake wa mkopo na vigogo wa Bundesliga, Borussia Dortmund kumalizika na tayari ameanza mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa 2024/25 akiwa na Manchester United. Nyota huyo raia wa England ambaye awali zilikuwa haziivi na Meneja Eric Ten Hag sasa mambo ni shwari baada ya kukutana na kumaliza sintofahamu iliyokuwa katikati yao.