Tue, 3 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa bara la Asia kati ya Al-Ittihad dhidi Sepahan nchini Iran umesitishwa kwasababu sanamu ya Jenerali wa Iran Qasem Soleimani (kamanda Mkuu wa kupambana na ugaidi) ilikuwa uwanjani.
FA ya Saudi imeamuru Al-Ittihad na Al-Hilal warejee nyumbani Saudi Arabia.
Al Ittihad tayari wamekwea pipa kurejea nchini kwao, huki Al Hilal ambao ilibidi wacheze mchezo wa Ligi hiyo siku ya kesho dhidi ya Nassaji Mazandaran nao wanatarajia kuanza safari ya kurejea kwao muda wowote kuanzia sasa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live