Mon, 3 Jun 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amepewa heshima ya jina lake kuitwa moja ya mitaa jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wamelazimika kumpa heshima hiyo Samatta kutokana na heshima anayoipa nchi kwenye soka.
"Tulimuita na kuzungumza naye, amepokea taarifa hivi kwa furaha na mchakato kwa ajili ya kuzindua mtaa huo inaendelea," alisema Makonda.
Alisema mtaa huo utakuwa manispaa ya Temeke na utazinduliwa baada ya Taifa Stars kurejea kutoka katika Afcon.
Chanzo: mwananchi.co.tz