Victor Osimhen alishindwa kutamba mbele ya Mbwana Samatta mwaka 2018/2019 wakati huo Samatta akiitumikia KCR Genk ligi kuu Nchini Ubelgiji, ukiwa ni msimu wake wanne katika Ligi ile wakati huo akiwa na umri wa miaka 27.
Msimu huo pia ndio msimu ambao Victor Osimhen alijiunga na Club ya Sporting Charleroi kwa mkopo akitokea VFL Wolfsburg ya Ujerumani akiwa na miaka 21.
Samatta alifunga magoli Ishirini (20) msimu wa mwaka 2018/19 akiisaidia KCR GENK kutwaa taji la Ligi kuu Nchini Ubelgiji (Belgium Pro League) kwa alama 63 huku Sporting Charleroi wakishika katika nafasi ya Sita wakiwa na alama 42.
Osimhen alifunga magoli 12 akishika nafasi ya Saba katika msimamo wawafungaji bora katika ligi hiyo ambapo Samatta alishika nafasi ya kwanza akiwa na goli zake 20 net.