Mon, 22 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars ) Mbwana Ally Samatta akizungumza mara baada ya mchezo wa Kundi F wa AFCOn kumalizika kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Zambia.
"Matokeo ndiyo kama hivyo, kuna wakati ulifika tukawa tunaamini kama tutapata ushindi lakini mechi haikuwa imeisha. Mechi imeisha na sare ya 1-1 kwa hiyo inabidi tuchukue.
"Hatuwezi kubadilisha chochote mechi imeshaisha, tuna mchezo mmoja mkononi inabidi tupambane kupata ushindi ili tuone kama tunaweza kusonga mbele," amesema Samatta.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live