Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Salah kuvunja rekodi ya Ronaldo Saudi Arabia

Mo Salah 2 Mohammed Salah

Sun, 27 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

AL-Ittihad ya Saudi Arabia imeripotiwa kuwa na uhakika wa kunasa saini ya supastaa wa Liverpool, Mohamed Salah kabla ya dirisha la kufungwa. Na kama dili hilo litatiki, basi Mo Salah atakuwa mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani, akimpiku kwa mshahara, supastaa wa Kireno, Cristiano Ronaldo.

Al-Ittihad ipo tayari kumpa winga huyo wa Misri ofa ya mshahara itakayozidi ule anaolipwa Ronaldo huko Al-Nassr wa Pauni 173 milioni, huku wakilenga kuwalipa Liverpool ada ya uhamisho ya Pauni 86 milioni.

Kwa sasa, Ronaldo, ndiye mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani, huku akifanywa kama nembo ya Saudia. Dili la mkali huyo wa zamani wa Manchester United linamshuhudia akilipwa Pauni 3.4 milioni (Sh 10.7bilioni) kwa wiki na atakuwa anakunja mkwanja huo hadi Juni 2025.

Lakini, kama Mo Salah atatua Saudia, basi atavuna pesa nyingi kuzidi mastaa wote. Na kinachoelezwa, klabu hiyo ya Saudia ina uhakika itanasa saini ya staa huyo kwenye umri wa miaka 31 kabla ya dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi kufungwa.

Mwandishi wa habari, Rudy Galetti alisema: “Al Ittihad hawatakata tamaa kwa Salah. Wametuma ofa kubwa sana kumshawishi hasa Klopp (Jurgen) ambaye bado anapingana na ishu ya kumuachia aondoke.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live