Baada ya ushindi wa Liverpool wa mabao (2-0) dhidi ya Everton ,Juzi Jumamosi Mohamed Salah anakuwa mchezaji wa kwanza wa Kiafrika kufunga magoli 145 katika Ligi Kuu ya Uingereza hii ni baada ya kufunga mabao mawili peke yake .
Tangu kuanza kwa mwaka huu 2023 tayari amehusika kwenye magoli zaidi ya 30+ kwenye ligi kuu Uingereza EPL
31 Mechi
19 magoli
12 assist
Mbali na hapo Salah amefanikiwa kufikisha mabao 201 kwenye maisha yake ya soka la kulipwa akicheza kwenye ligi kuu mbali mbali [ Magoli ya Ligi kuu tu]
Mechi 13 zilizotangulia akiwa katika uwanja wa Anfield amefunga au kutoa assist kwenye mechi zote (Asipokufunga basi atatoa assist)
Idadi ya magoli ya jumla aliyofunga kwenye uwanja wao Anfield ni 104 hii ni sawa na Kenny Dalglish na Steven Gerrard (Magoli ya jumla Anfield)