Fri, 24 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Simba Pape Ousmane Sakho anazidi kujisafishia jina tangu kuitwa katika kikosi cha Timu ya Taifa ya Senegal.
Sakho tangu aitwe katika kikosi hicho amekuwa burudani kwa nyota wenzake wa Kikosi hicho ambao wengi wao wanacheza Ligi za Bara la Ulaya.
Tayari Sakho ameshatokea katika ukurasa wa Sadio Mane na ukurasa wa Timu ya Taifa ya Senegal na huenda ikawa sababu ya kutazamwa kwa karibu na Mawakala wakubwa wa Soka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live