Tue, 14 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la soka nchini TFF limetoa taarifa ya kufungiwa kwa klabu ya Singida Fountain Gate kufanya usajili kutokana na kushindwa kumlipa malimbikizo ya mshahara nyota wake raia wa Ghana Asamoah Gyan.
Baada ya taarifa hiyo kutoka Afisa habari wa klabu hiyo Hussein Massanza amesema tayari kama klabu wameshamalizana na nyota huyo itakuwa TFF imechelewa kutoa taarifa hiyo.
"Naona taarifa itakuwa imechelewa kidogo Gyan tumeshamalizana nae!".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live