Tue, 16 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ofisa habari wa Coastal Union, Abbas El Sabri amesema, klabu hiyo imepokea wito wa kamati ya sheria na hadhi za wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa ajili ya kusikiliza shauri la mchezaji wao Lameck Lawi ambalo litasikilizwa leo Julai 16, 2024.
Coastal na Simba zimeingia kwenye mgogoro wa kumgombania beki Lameck Lawi Simba ikimtangaza kama mchezaji wao na Coastal ikisema mchezaji huyo hajauzwa bado ni mali ya Coastal.
Aidha Sabri amesema wako tayari kupambania haki Yao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live