Sun, 18 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Arsenal imeibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya wenyeji, Burnley katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Jumamosi Uwanja wa Turf Moor mjini Burnley.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Martin Odegaard dakika ya nne, Bukayo Saka mawili dakika ya 41 kwa penalti na 47, Leandro Trossard dakika ya 66 na Kai Havertz dakika ya 78.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 55, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi mbili na Liverpool baada ya wote kucheza mechi 25, wakati Burnley inabaki na pointi zake 13 za mechi 25 nafasi ya 19.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live