Safu ya ulinzi ya kikosi cha Yanga inayoongozwa na Bakari Nondo Mwamnyeto, Dickson Job na Ibrahim Hamad Bacca ndiyo imeongoza kwa kuruhusu mabao mengi zaidi miongoni mwa timu nane ambazo zimefuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Yanga ambayo imeruhusu mabao sita kwenye hatua ya makundi, ilifungwa mabao matatu na CR Belouizdad (ugenini), ikaruhusu bao moja dhidi ya Medeama (ugenini), bao moja dhidi ya Al Ahly (nyumbani) na bao moja dhidi ya Ahly tena ugenini.
1. Petro de Luanda - bao 0
2. Mamelodi Sundowns - bao 1
3. Ahly Ahly - bao 1
4. ASEC Mimosas - bao 2
5. Simba Sc - bao 2
6. TP Mazembe 2
7. Esperance - bao 3
8. Yanga Sc - bao 6.
Unadhani nani alaumiwe?