Sat, 3 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars" sasa ni rasmi imetupwa nje katika kinyang'anyiro cha kuwania kufuzu kwa michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN, baada ya kukubali kichapo cha magoli 3-0 kutoka kwa Uganda jioni hii.
Ushindi huo wa Uganda unawafanya kujihakikishia ushindi wa jumla wa magoli 4-0 baada ya mchezo wa awali uliopigwa Jijini Dar es Salaam Stars kukubali kichapo cha goli 1-0 kipigo kilichomuondoa Kocha Kim Poulsen.
Magoli ya Uganda katika mchezo wa leo yamefungwa na Moses Waisa kwa mkwaju wa penati, Basangwa (52) na Rodgers (75).
Chanzo: www.tanzaniaweb.live