Fri, 25 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Azam FC imetolewa katika Kombe la Shirikisho Afrika kwa penati 4-3 dhidi ya Bahir Dar Kenema ya #Ethiopia kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.
Azam FC iliongoza magoli 2-1 katika dakika 90 lakini matokeo ya jumla yakawa 3-3, hivyo mechi ikaelekea kwenye matuta.
Waliofunga penati za Azam FC ni Yannick Bangala Litombo, Feisal Salum ‘Fei Toto’ na Cheikh Sidibé wakati waliokosa ni Djibril Sylla, Sospeter Bajana na Idris Mbombo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live