Mon, 25 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ofisa Habari wa Singida Fountain Gate FC, Hussein Massanza ameeleza kuwa kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefutia kadi nyekundu aliyoonyeshwa Thomas Ulimwengu kwenye mchezo dhidi ya Namungo FC.
Hatua hiyo n baada ya kujiridhisha kupitia Ushahidi wa picha jongeo (video) na taarifa za wakufunzi wa waamuzi kuwa hakustahili adhabu hiyo kwa kosa alilotenda.
Adhabu hiyo ni kwa kuzingatia Kanuni ya 12:8 ya Ligi Kuu kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live