Fri, 4 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ruvu Shooting walilazimishwa sare ya 1-1 na Mbeya Kwanza Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
Saadat Mohamed alianza kuifungia Ruvu Shooting dakika ya 36, kabla ya Habib Kyombo kuisawazishia Mbeya Kwanza dakika ya 51.
Kwa matokeo hayo, Ruvu Shooting inafikisha pointi 12 na kusogea nafasi ya 14 na Mbeya Kwanza wanatimiza pointi 13, ingawa wanabaki nafasi ya 12 baada ya tlmu zote kucheza mechi 14.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live