Wed, 3 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na England, Wayne Rooney amefutwa kazi kama kocha mkuu wa klabu ya Birmingham City kufuatia mwenendo usioridhisha wa matokeo tangu ajiunge na klabu hiyo.
Rooney (38) ameiongoza Birmingham kwenye mechi 15 akipoteza mechi 9, sare 4 na ushindi mara mbili (2) tu.
Klabu hiyo imeporomoka kutoka nafasi ya 6 mpaka nafasi ya 20 kwenye msimamo wa Championship ndani ya siku 83 za utumishi wa Rooney kama kocha Mkuu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live