Wed, 21 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Wayne Rooney, amesema mfungaji bora wa kombe la Dunia Kylian Mbappe kuendelea kusalia ndani ya PSG sio uamuzi sahihi, badala yake ajiunge na Manchester United au Real Madrid .
"Mbappe ni mchezaji mzuri lakini PSG hapamfai , nadhani anapaswa kwenda klabu kama United au Real Madrid " amesema Rooney
Kauli hiyo ya Rooney huenda ikawakasirisha mabosi wa PSG kwani walifanya kila jitihada mwishoni msimu uliopita kumbakisha Mbappe klabuni hapo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live