Fri, 18 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Manchester United imechukua hatua za awali za kumfuta kazi mshambuliaji Cristiano Ronaldo kufuatia mahojiano yake na mwandishi Piers Morgan.
Ronaldo anashutumiwa kuvunja masharti ya mkataba wake hivyo mkataba utavunjwa na anatarajiwa kupoteza kiasi cha pauni milioni 16 (Tsh bilioni 41) za mishahara.
Mreno huyo hana nafasi ya kurejea tena klabuni hapo huku wachezaji wenzake wakiripotiwa kuwa na maoni tofauti juu ya mshindi huyo mara 5 wa Ballon d'or.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live