Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ronaldo kuongoza All-Star XI katika mechi ya kirafiki dhidi ya Messi

Ronaldo Messi Saudi Ronaldo kuongoza All-Star XI katika mechi ya kirafiki dhidi ya Messi

Tue, 17 Jan 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mshambuliaji bora kila wakati Cristiano Ronaldo anatazamiwa kuongoza timu ya Saudi All-Star XI dhidi ya PSG katika mechi yao ya kirafiki siku ya Alhamisi, Januari 19.

Mechi hiyo itakuwa ya kwanza kwa Ronaldo kushiriki tangu ajiunge na Al-Nassr mnamo Disemba 2022 kwa mkataba wa miaka miwili.

Tayari Ronaldo amekabidhiwa jukumu la kukiongoza kikosi chake ambacho kitakuwa na wachezaji wa Al-Nassr na Al-Hilal.

Ronaldo amekabidhiwa cheo cha unahodha, na sasa zimesalia siku chache tu aanze kusakata dimba kwa mara ya kwanza nchini Saudi Arabia.

Mechi hiyo vile vile itamkutanisha Ronaldo na hasimu wake wa muda mrefu Lionel Messi, ambaye atakuwa ananogesha kikosi cha PSG ambao kwa sasa wako safarini kuelekea katika taifa la Mashariki ya Kati.

Mabingwa Ronaldo na Messi walikuwa na ushindani mkali wakati walipokuwa pamoja nchini Uhispania, wakichezea Real Madrid na Barcelona mtawalia.

Ronaldo aliondoka Uhispania na kujiunga na Juventus mwaka wa 2018, na hajamenyana na Messi tangu Disemba 2020 wakati wababe hao wa Italia waliposafiri hadi Nou Camp.

Messi ahusishwa na klabu ya Saudi Arabia Ripoti ziliibuka kuwa mchezaji huyo nyota mwenye umri wa miaka 35, ameviziwa na ofa ya mamilioni kujiunga na klabu ya Al-Hilal, kulingana na Barca Universal.

Hata hivyo, mtaalam wa soka wa Uhispania Guillem Balague alipuzilia mbali madai hayo akisema Messi hana hamu ya kuhamia Saudi Arabia. Tangu kushinda Kombe la Dunia nchini Qatar mwezi uliopita, Messi amejiwekea malengo mapya kama Balague anavyodai.

Mkataba wake wa sasa na Les Parisiens utakatika msimu huu wa joto lakini ripoti ziliibuka kuwa alirefusha muda wake Ufaransa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live