Tue, 4 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Inter Miami imepanga kuanza harakati za kuangalia uwezekano wa kumsajili nahodha wa klabu ya Al Nassr Riyadh, Cristiano Ronaldo.
Timu hiyo ya Inter Miami kutoka Marekani inataka kumsajili mchezaji huyo katika dirisha kubwa la usajili.
Kama usajili huo utakamilika Ronaldo ataenda kukutana na hasimu wake wa muda mrefu Lionel Messi ambaye anakipiga katika klabu hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live