Wed, 15 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Al Nassr FC ya Saudi Arabia imefungua mazungumzo na nyota wa Ureno, Cristiano Ronaldo juu ya nyongeza ya mkataba mpya wa kuendelea kusalia klabuni hapo mpaka 2027.
Mkataba huo mpya unatarajiwa kuanza Januari 2025 na kutamatika Januari 2027.
Hivyo Ronaldo anaweza kupata nafasi ya kushiriki kombe la Dunia 2026 akiwa mchezaji wa Al Nassr FC.
NB: Mkataba huo mpya wa Ronaldo utamalizika mwezi mmoja kabla ya mshindi huyo mara 5 wa Ballon d'or kutimiza miaka 42.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live