Mon, 5 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Cristiano Ronaldo amekubali dili la TZS bilioni 494 kwa msimu na Al-Nassr FC ya Saudi Arabia.
Ronaldo ambaye ni mchezaji huru anatarajiwa kujiunga na klabu hiyo Januari 2023 kwa mkataba wa miaka miwili na nusu, hivyo kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa ghali zaidi duniani.
Hivi karibuni, Ronaldo aliingia kwenye mvutano na kocha wake Ten Hag wa Man U ambapo Ronaldo aliwasema vibaya Man U kwenye mahojiano yake ambayo yalizua gumzo na mwishoni uongozi wa timu hiyo ulimalizana naye kwa makubaliano ya pande zote mbili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live