Mshambuliaji wa Al Nassr, Cristiano Ronaldo ametuma msaada wa vitu katika nchi za Syria na Uturuki kufuatia tetemeko la ardhi lililosababisha vifo zaidi ya 50,000 na kusababisha hasara kubwa kwa nchi hizo.
Mshambuliaji wa Al Nassr, Cristiano Ronaldo ametuma msaada wa vitu katika nchi za Syria na Uturuki kufuatia tetemeko la ardhi lililosababisha vifo zaidi ya 50,000 na kusababisha hasara kubwa kwa nchi hizo. Ronaldo ametuma shehena ya ndege ya vitu vya kuwahudumia wahanga ikiwa pamoja na mahema, vifurushi vya chakula, mito, blanketi, vitanda, vyakula vya watoto, maziwa na vifaa vya matibabu.