Baada ya Neymar Jr. kumwaga chozi hapo juzi wakati timu yake ya Brazil ikiondolewa na Croatia jana Jumamosi, Desemba 10, 2022 imekuwa zamu ya Cristiano Ronaldo.
Ureno imepokea kichapo kutoka kwa Simba wa Atlas, Morocco nahivyo kuondolewa katika michuano hiyo.
Morocco imeweka rekodi kwa mara ya kwanza ya kuwa timu pekee kutoka Afrika kuingia hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia.
Bao la pekee limefungwa na Yusuf En Nesyri dakika ya 42.
Tangu kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1930 Morocco inakuwa timu ya kwanza kutoka Afrika kuingia nusu fainali ya mashindano hayo. Timu hiyo sasa itakutana na mshindi wa England na Ufaransa.