Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ronaldo akwama kwenda Qatar

Cr 7 Qatar Ronaldo akiwa haamini baada ya kupoteza mbele ya Serbia

Mon, 15 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Nyota Cristiano Ronaldo jana alishindwa kuisaidia Ureno kupata nafasi ya kucheza Kombe la Dunia baada ya kuchapwa 2-1 nyumbani na Serbia Uwanja wa Luz Jijini Lisbon.

Renato Sanches aliyeanza badala ya Bruno Fernandes aliifungia bao la kuongoza Ureno dakika ya pili, kabla ya Dusan Tadic kuisawazishia Serbia dakika ya 33 na Aleksandar Mitrovic kufunga la ushindi dakika ya 90.

Serbia inamaliza na pointi 20 kileleni kwa Kundi A na kufuzu moja kwa moja Kombe la Dunia, mwakani wakati Ureno ya Cristiano Ronaldo iliyoshika nafasi ya pili kwa pointi zake 17 itakwenda Play-Offs kujaribu bahati ya kucheza Qatar 2022.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live