Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ronaldo: Nilikaribia kujiunga na Man City lakini kuna mtu alinizuia

Ronaldo Ferguson Cristiano Ronaldo

Thu, 17 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Cristiano Ronaldo anasema alikuwa karibu kujiunga na Manchester City kabla ya kufuata "moyo" wake kwa kujiunga tena na Manchester United.

Fowadi huyo wa Ureno aligonga vichwa vya habari mapema wiki hii baada ya kuiambia Talk TV kuwa anahisi "amesalitiwa" na klabu hiyo.

Sehemu ya kwanza ya mahojiano kamili ilitolewa Jumatano ambapo alitoa maelezo zaidi juu ya toleo lake la matukio huko Old Trafford.

"Kusema kweli, ilikuwa karibu," alisema kuhusu uwezekano wa kujiunga na City.

Ronaldo alirejea Old Trafford akitokea Juventus mnamo Agosti 2021 - miaka 11 baada ya kuihama klabu hiyo na kujiunga na Real Madrid.

Wakati huo iliripotiwa kutakiwa na kocha wa City Pep Guardiola na ingawa Ronaldo alithibitisha nia hiyo, alisema aliamua kusaini na United baada ya kuzungumza na meneja wake wa zamani Sir Alex Ferguson.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 aliongeza: "Kama unavyojua, historia yangu katika Manchester United, moyo wako, unahisi jinsi ulivyokuwa hapo awali, inaleta mabadiliko. Na bila shaka, Sir Alex Ferguson.

"Nilizungumza naye. Aliniambia, 'haiwezekani wewe kuja Manchester City'. Nami nasema 'Sawa, bosi'."

Ronaldo, ambaye atakosa mechi ya kirafiki ya Ureno dhidi ya Nigeria siku ya Alhamisi kwa sababu ya ugonjwa wa tumbo, alikosoa tabia na taaluma ya wanasoka chipukizi wakati wa mahojiano, akiwashutumu "kutowaheshimu" wachezaji wenzao wakubwa na wenye uzoefu zaidi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live