Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Roberto Firmino ageukia uchungaji

Firmino Robeto.jpeg Roberto Firmino ageukia uchungaji

Tue, 9 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Gwiji wa soka wa Liverpool, Roberto Firmino ametangaza kuwa mchungaji wa kanisa la kiinjilisti.

Nyota huyo wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazil aliwekwa wakfu katika kanisa lililoanzishwa katika mji aliozaliwa wa Maceio, Jumapili iliyopita, Juni 30.

Katika chapisho la pamoja kwenye Instagram, staa huyo mwenye umri wa miaka 32 na mkewe Larissa walielezea hafla hiyo kama "ya kukumbukwa na isiyoweza kusahaulika".



Pia waliongeza: “Kutokana na kukutana kwetu na Kristo, hamu inawaka mioyoni mwetu, ili watu wajue upendo huu ambao umetufikia. Sasa tuna shauku na wajibu mwingine kuwa wachungaji wanaoupendeza moyo wa Mungu na wanaoshirikiana na Ufalme."

Hapo nyuma mnamo 2020, mshambuliaji huyo alibatizwa kwenye bwawa la kuogelea kwenye nyumba ya mchezaji mwenzake wa zamani Alisson.

Mwanasiasa huyo wa zamani wa Hoffenheim mara nyingi hushiriki ujumbe wa kidini kwenye ukurasa wake na sehemu ya jumbe zake akihubiri.

Mnamo 2023 mchungaji huyo alijiunga na Al-Ahli ya Saudi Pro League na tangu wakati huo amecheza mechi 34 na kufunga mabao tisa.



Mshindi huyo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya 2021-22, aliichezea Liverpool kwa miaka minane na kuunda safu ya ushambuliaji ya ajabu akiwa na Mohamed Salah na Sadio Mane.

Wakati akiwa katika klabu hiyo, Mbrazil huyo pia alishinda Ligi Kuu, Kombe la FA na Kombe la EFL.

Kwa taifa lake, aliichezea Brazil mechi 55 na ndiye Mbrazil aliyefunga mabao mengi zaidi kwenye Ligi Kuu akiwa amefunga mabao 82.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live