Kocha Mkuu wa Simba SC, Roberto Oliviera 'Robertinho' amezungumzia droo ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo imefanyika jana.
Robertinho amesema anawaheshimu wapinzani atakaokutana nao kati ya Africans Stars au Power Dynamos lakini anajivunia kwa sasa anacho kikosi kipana na kizuri.
"Kwa kweli najivunia kuwa na kikosi imara, benchi zuri la ufundi. Mimi nafikiria vikubwa na Simba ni kubwa. Niwaombe mashabiki waisapoti timu kwani wao ndiyo wachezaji wa kumi na mbili, tujivunie Simba," alisema Robertinho.
Kocha Robertinho amezungumzia droo ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo imefanyika leo ambapo Simba hatutacheza hatua ya awali lakini katika hatua ya kwanza tutakutana na Africans Stars au Power Dynamos.
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) July 25, 2023
Kuangalia mahojiano kamili ingia kwenye Simba App. #NguvuMoja pic.twitter.com/7wgS35ewvz