Thu, 19 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Simba SC, Roberto Oliviera 'Robertinho' amesema, anamheshimu mpinzani wake wa Al Ahly katika mchezo wa African Football League lakini watapambana washinde.
Robertinho ameyasema hayo alipokuwa kwenye mahojiano ya wanahabari kuelekea mchezo huo wa kesho.
"Tunafahamu tunacheza na timu kubwa lakini na sisi ni timu kubwa, naamini kikosi na uwezo wa wachezaji wangu naamini kesho tutashinda," alisema Robertinho.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live