Mon, 28 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Katika mchezo dhidi ya RS Berkane wakati ubao wa Municipal de Berkane ukisoma RS Berkane 2-0 Simba rekodi muhimu ziliwagomea Simba huku ile mbovu ikijibu.
Simba walifanikiwa kucheza jumla ya faulo 19 huku wapinzani wakicheza faulo 8 na ni kadi za njano moja tu kwa RS Berkane na 5 zilikuwa kwa nyota wa Simba.
Miongoni mwa nyota wa Simba ambao walionyeshwa kadi za njano ni pamoja ma Berkane Morrison, Joash Onyango, John Bocco.
Katika safu ya ushambuliaji ni mashuti mawili yalipigwa na Simba nayo hayakulenga lango huku RS Berkane wakipiga mashuti 19 na ni mashuti 5 yalilenga lango.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live