Kikosi cha Yanga leo kitashuka Dimbani dhidi ya JKT Tanzania katika Mchezo wa Mzunguko wa 23 Ligi Kuu Tanzania Bara.
JKT inaenda kukumbana na Yanga ikiwa na historia isiyofurahisha kwa Wapenzi wa Klabu hiyo kwani Mchezo wa Kwanza Walipoteza kwa Kufungwa goli 5 kwa sifuri.
Mchezo huo Utachezwa katika Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni Mkoani Dar es Salaam Majira ya 10:00 Jioni.
Michezo Waliowahi Kucheza:-
2018 Yanga 3-0 JKT Tanzania
2019 JKT Tanzania 0-1 Yanga
2019 Yanga 3-2 JKT Tanzania
2020 JKT Tanzania 1-1 Yanga
2021 Yanga 1-0 JKT Tanzania
2023 Yanga 5-0 JKT Tanzania
JKT Tanzania ni Miongoni mwa timu zinazo tazamiwa Kushuka Daraja Msimu huu wa 2023/24 Kwani ni badala wa Mwisho Ikiwa Imecheza michezo 22 imefunga goli 16 ikiwa nafasi ya 15 kati ya 16.