Nyota wa zamani wa klabu ya AS Roma ambaye kwasasa ni kocha kwenye klabu ya Fiorentina Alberto Aquilan ameweka wazi kuwa siku ya kwañza kuanza kuichezea AS Roma aliingia dakika ya 90 na mwamuzi akampa nafasi ya upendeleo.
"Nakumbuka mechi yangu ya kwanza ya Serie A, tulikuwa tunaongoza goli 3-1 na nikaingia dakika ya 90."
"Ndani ya dakika tatu tangu niingie sikuugusa mpira hata mara moja, refa akaniambia 'usijali sitapuliza kipyenga hadi uuguse mpira'.
"Kwahiyo mchezo ukawa umekula dakika nyingi tofauti ilivyokuwa inahitajika, lakini hatimae nikawa nimeugusa mpira."
Alberto Aquilani akieleza siku yake ya kwanza kupata nafasi ya kuitumikia AS Roma kwenye mchezo wa Ligi ya Serie A.