Huko Mexico mwamuzi Fernando Hernandez kafungiwa mechi 12 kwa kumpiga mchezaji kifuti cha kwenye kinena.
Kiungo Lucas Romero na wachezaji wenzake wa Leon walimzonga mwamuzi wakihitaji akiajiridhishe kwanza katika VAR baada ya wapinzani wao Club America kufunga goli la kusawazisha la utata katika Ligi ya Mexico.
Mwamuzi Hernandez ambaye tayari alishatoa adhabu kwa wachezaji wenzake na Romero aliinua goti lake na kumpiga Romero sehemu za siri baada ya kufokewa na Romero.
Kilichofuata ni Romero kuanguka chini huku akiugulia kwa maamuzi makali.
Rodillazo del árbitro al jugador de León, esto le puede costar la carrera a Fernando Hernandez, Archundia como explicas esto, agresión del árbitro. pic.twitter.com/QzOjGxwpbg
— Felipe Ramos Rizo (@ramosrizo) April 2, 2023