Sat, 4 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa Al Ahly Sporting Club, Reda Slim huenda akawa nje ya Dimba Kwa muda wa miezi mitatu baada ya kupata majeraha katika mchezo wa African football League dhidi ya Mamelodi Sundowns.
Nyota huyu aliumia Bega baada ya kukutana na beki mgumu Khuliso Mudau ambaye alimzidi ujanja ndipo Reda Slim akaamua kumdanganya mwamuzi Kwa kujiangusha.
Janja yake hii ilimfanya atue vibaya na Bega lake la kushoto likapata hitilafu.
Reda Slim tayari alikuwa ameingia katika mfumo wa timu hii ila kukutana na Khuliso Mudau kulimfanya Winga huyu apate Wakati mgumu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live