Kikosi cha Yanga leo kimesafiri kuelekea Afrika Kusini kwaajili ya kucheza michezo mbali mbali ya kirafiki kuanzia tarehe 20 ambapo watacheza na FC Augsburg, TS Galaxy na Kaizer Chiefs
Ofisa habari wa Yanga, Ally Kamwe akizungumza wakati timu yake ikisafiri kuelekea Afrika Kusini amesema Yanga watashiriki Mpumalanga Cup ambapo watacheza na timu kutoka Ujerumani, lakini pia watacheza Toyota Cup kwa mwaliko wa timu ya Kaizer Chiefs kabla ya kurejea nchini kwenye wiki ya Mwananchi na Ngao ya jamii.
July 20 vs Ausburg
July 28 vs Kaizer Chiefs.
August 04 Wiki Ya Mwananchi
August 08 vs Simba SC
August 16 vs Vital'O FC
August 23 vs Vital'O FC
Young Africans Sports Club wameondoka nchini 18 July 2024 (keshokutwa) kuelekea nchini Afrika Kusini.
Ratiba ikienda vizuri wamepanga kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Augsburg SC ya ligi kuu ya Ujerumani 20-21 July 2024.
Pia, watacheza mechi ya Toyota cup dhidi ya klabu ya Kaizer Chiefs 28 July 2024.