Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ratiba, mechi za UEFA Champions League

Uefa Ratiba Mechi za UEFA, Septemba 28

Tue, 28 Sep 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ni vita ya kusaka pointi 3 muhimu kwa kila timu katika kuhakikisha wanaweka mazingira mazuri ya kusonga hatua ya 16 bora.

Usiku wa leo Septemba 28 kutakuwa na mechi nane za Ligi ya Mabingwa barani Ulaya huku pia vigogo kadhaa wakishuka dimbani.

Real Madrid watakuwa nyumbani katika mchezo wa kundi D kuwakaribisha klabu ya FC Sheriff, huku Shakhtar wakiwakaribisha Inter Milan kutoka Italia.

Katika michezo ya kundi B, liverpool watakua ugenini kule Ureno kupepetana na Porto huku AC Milan wakiwakaribisha Atletico De Madrid.

Mchezo unsosubiriwa kwa hamu ni ule wa PSG dhidi ya Manchester City ambao utapigwa majira ya saa nne za usiku katika Uwanja wa Parc De Princes.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live