Sun, 24 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi kuu Tanzania Bara (NBC Primia Ligi) inaendelea leo Oktoba 24 kwa michezo miwili.
Katika Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani, Ruvu Shooting wataikaribisha Polisi Tanzania majira ya saa 10:00 jioni.
Mchezo mwingine ni kule katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma ambapo wenyeji Dodoma Jiji wataikaribisha timu ya maafande wa Tanzania Prisons.
Mchezo huo utapigwa majira ya saa 1:00 usikubaada ya ukarabati wa uwanja na kufungwa taa, zinazoruhusu michezo kuchezwa usiku.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live