Tue, 30 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2021/2022 itaendelea leo kwa mechi tatu ambapo timu zitaumana kwa dakika 90.
Kule katika Mkoa wa Mara Biashara United watawakaribisha maafande wa Polisi Tanzania majira ya saa 10:00 jioni.
Kule Jijini Mbeya katika uwanja wa Kumbu Kumbu ya Sokoine, Vinara wa Ligi Yanga watavaana na Mbeya Kwanza majira ya Saa 10:00
Mchezo wa mwisho siku ya leo ni pale Chamazi Complex ambapo wana lamba lamba Azam FCwatawakaribisha Mtibwa Sugar mchezo utakaochezwa majira ya saa 1:00 usiku
Chanzo: www.tanzaniaweb.live