Sun, 12 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2021/2022 (NBC Primia Ligi) inaendelea leo kwa michezo miwili.
Vibonde katika Ligi hiyo timu ya Mtibwa Sugar itakuwa kule Manungu Mkoani Morogoro kuwakaribisha wanajeshi wa Mpakani, Timu ya Biashara United majira ya saa 10:00 jioni.
Mchezo wa Pili ni Matajiri wa Jiji Azam FC ambao watakua nyumbani Kule Azam Complex kuwakaribisha Kagera Sugar majira ya saa 1:00 usiku
Tazama hapa chini ratiba ya michezo ya leo;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live