Tue, 19 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ni usiku wa Ulaya, ambapo vilabu kadhaa vitashuka dimbani kusaka alama tatu katika michezo ya hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League).
Wababe kutoka England klabu ya Liverpool, watasafiri mpaka kule nchini Hispania kwenda kupepetana na vijana wa Diego Simeone, Atletico Madrid.
Wakati Manchester City watakuwa wageni wa Club Brugge, wababe kutoka Ufaransa klabu ya PSG watavaana na Leipzig pale Parc de Princes.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live