Sasa ni rasmi timu za Yanga SC, Simba SC, Azam FC na Singida Big Stars ndiyo zitaiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya CAF. Ikiwa timu mbili kwenye CAF Champion League na Timu mbili kwenye CAF Confederation Cup
Hii inatokana na timu zote nne (Yanga, Simba, Azam, Singida) kufanikiwa kufuzu nusu fainali ya kombe la shirikisho (Azam Sports Confederation Cup). Pia Timu hizo zipo nne bora kwenye msimamo wa ligi kuu ya NBC.
Timu ya Geita Gold FC inashika nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi ya NBC ina pointi 34 haiwezi kuifikia Timu ya Azam FC inayoshika nafasi ya 4 ikiwa na pointi 50. Ikiwa Timu ya Geita imebakiza michezo 5 (34+15= 49).