KLABU ya Yanga imemtambulisha rasmi golikipa wao mpya, Aboutwalib Hamidu Mshery ambaye amesajiliwa katika dirisha hili dogo la usajili akitokea Mtibwa Sugar.
Utambulisho huo umefanyika leo Jumatano, Desemba 29, 2021 ambapo Klabu ya Yanga kupitia kurasa rasmi za mitandao yake ya kijamii imeposti picha zinazoonekana na kuandika "Aboutwalib Hamidu Mshery is now Green & Yellow???? @_mshery ????????
" Karibu kwa #wananchi ????✍???????? @_mshery #daimambelenyumamwiko
Mshery ametua Jangwa kwenda kuchukua mikoba ya aliyekuwa kipa wao namba mbili, Ramadhani Kabwili ambaye ameachwa na klabu hiyo inayoongoza Ligi Kuu Tanzania Bara kwa sasa.