Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rasmi: KMC yamruhusu Awesu kujiunga na Simba

Awesu Asx Awesu Awesu

Thu, 15 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya KMC imethibitisha kufikia makubaliano na Simba SC juu ya uhamisho wa mchezaji Awesu Ali Awesu ambaye awali KMC walimuwekea pingamizi kucheza Simba Sc kwa madai kuwa hakufuata taratibu za kuvunja mkataba.

Awali Awesu aliilipa KMC shilingi milioni 50 kama kipengele cha mkataba wake kilivyokuwa kinataka na kutangazwa kama mchezaji mpya wa Simba Sc.

Hata hivyo baada ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji kupitia pingamizi la KMC wakabaini nyota huyo hakufuata taratibu za kuvunja mkataba na kuamriwa kurudi kwa Waajiri wake wa zamani kabla ya suala hilo kufikiwa muafaka leo.

Kwa mujibu wa taarifa ya KMC, makubaliano hayo yamefikiwa baada ya vikao vya timu zote mbili.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live