AS Vita Club ya nchini Congo DR wametangaza rasmi kuipata saini ya kiungo mshambuliaji wa Kimataifa raia wa Mali, Aboubakar Diarra mwenyewe umri wa miaka 30.
Diarra amesaini mkataba wa miaka miwili akitokea Klabu ya Al Ittihad ya nchini Libya kama mchezaji huru baada ya mkataba wake kutamatika.
Kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Mali anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Dauphins Noirs ya Kinshasa ambao ndio wameanza usajili wao kwa ajili ya msimu ujao.
Vita Club wamedhamiria kufanya usajili wa nguvu msimu huu na kuingiza damu mpya kwenye kikosi chao baada ya kusuasua kwenye Ligi ya Congo na kushindwa kufanya vizuri kimataifa.
Kinshasa Black Dolphins sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye Kombe la Congo wakiwa na kikosi chao cha sasa, wakitarajia kupata nafasi ya kushiriki mashindano ya vilabu barani Afrika ambayo yatawawezesha wale wote wanaokuja kunufaika na ushiriki huu ambapo watalazimika kupambana ili kufika huko.