Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rashford anasa kwenye penzi la mrembo huyu

NHVHFFHFH Rashford anasa kwenye penzi la mrembo huyu

Wed, 1 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Gazeti la The Sun la nchini Uingereza limeibua tetesi za mchezaji wa klabu ya Manchester United, Marcus Rashford kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamitindo kutoka nchini Colombia, Erica Correa baada ya hivi karibuni kuonekana wakiwa pamoja katika kumbi za starehe.

Wawili hao wamekuwa gumzo mitandaoni ambapo baadhi ya watu wana hisi huwenda wakawa katika mahusiano ya kimapenzi.

Rashford mwenye umri wa miaka 26 alionekana akiwa na mwanamitindo huyo mzaliwa wa Colombia kwenye ukumbu wa starehe katika jiji la Manchester nchini Ungereza siku ya Jumapili jioni.

Inadaiwa kuwa nyota huyo wa Man United tangu alipoachana na mpenzi wake Lucia Loi mwaka 2023 hakuwahi kuonekana na mwanamke kwa ukaribu hivyo kama alivyo kuwa na mwanamitindo huyo.

Rashford na Lucia Loi walianza kuwa katika mahusiano miaka nane iliyopita wakiwa na umri wa miaka 15 wakiti wapo shule ya Aston iliyopo Manchester na kuachana mwaka 2023.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live