Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rashford, Ten Hag wayamaliza

Rashford X Ten Hag Fresh Rashford, Ten Hag wayamaliza

Thu, 1 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha wa Manchester United Erik Ten Hag amethibitisha kuwa klabu hiyo imemuwajibisha mshambuliaji wao Marcus Rashford kwa makosa ya kinidhamu wikiendi iliyopita, yameisha na sasa amejiunga na wenzake kwaajili ya mchezo wa ligi dhidi ya Wolves.

“Hatukuambatana naye jumapili (mchezo uliopita), yalikuwa ni masuala ya kinidhamu na ameshawajibishwa, mengine ni mambo ambayo yanatakiwa yaishie ndani ya timu, tutakuwa naye dhidi ya Wolves”

Rashford alikumbana na adhabu nzito ya kukatwa mshahara zaidi ya bilioni 2 za kitanzania baada ya kunaswa akiwa sehemu za starehe siku 1 kabla ya mchezo wa ligi wkiendi iliyopita.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live