Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rashford: Sijali mashabiki wanasema nini

Rashford.jpeg Marcus Rashford

Thu, 15 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mshambuliaji Marcus Rashford amesema amejitolea kikamilifu kwa silimia 100 kwa timu ya taifa ya England na hajali ikiwa kuna watu watamkosoa au kutilia shaka kujitolea kwake.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 anajiandaa kwa mechi ya kufuzu kwa Euro 2024 dhidi ya Malta na Macedonia Kaskazini baada ya kujiondoa kwenye kikosi hicho Machi kutokana na jeraha.

Rashford amelazimika kujiondoa katika kambi nyingi hivi karibuni lakini uamuzi wake wa kwenda New York wakati England waliposhinda mechi yao ya kwanza ya Kundi C 2-1 nchini Italia ulizua mjadala.

Gareth Southgate alitetea uamuzi wa mshambuliaji huyo mwenye mataji 51 kuelekea Marekani wakati huo na fowadi huyo wa Manchester United amesema hakuona tatizo.

“Sikuona, kuwa mkweli kwako,” alisema Rashford.

“Nahitaji muda wa kupona, kwa hiyo nilichukua safari fupi, siku nne, kisha nikarudi kufanya mazoezi na kujaribu tu kujiandaa haraka iwezekanavyo.

“Nashukuru nina matatizo machache ya misuli na aina ya majeraha, lakini mara kwa mara unapata majeraha. Mengi ya majeraha yangu yamekuwa hivyo.”

Alipoulizwa ikiwa watu wanaohoji kujitolea kwake kwa nchi yake, Rashford alijibu: “Kusema kweli, sivyo wanavyofikiri.

“Ninajua kuwa nimejitolea kwa asilimia 100, watu watasema kile watakachosema, hainisumbui sana.”

England inajianda kucheza mechi ya kufuzu Euro 2024 dhidi ya Malta kesho Ijumaa kabla ya kuwavaa Macedonia Kaskazini Jumatatu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: